TAFRANI MV. MAGOGONI KIGAMBONI TANZANIA

DARA ES SALAAM
Wananchi wa Wilaya ya Kigamboni na maeneo mengine jijini Dar es Salaam leo wamekumbwa na taharuki baada ya Kivuko cha MV Magogoni kupata hitilafu na kupoteza mwelekeo hali iliyosababisha kupumzishwa kwa takribani saa mbili na kuongeza tatizo la usafiri kati ya Kigamboni na Feri.
Wananchini wa Wilaya ya Kigamboni na maeneo mengine jijini dar es salaam leo wamekubwa na Taharuki baada ya Kivuko cha MV Magogoni kupata hitilafu na kupoteza mwelekeo hali iliyosababisha kupumzishwa kwa takribani saa mbili na kuongeza tatizo la usafiri kati ya Kigamboni na Feri.
Hali hiyo ilisababisha msongamano mkubwa wa abiria na magari hasa kutokana na kulazimika Kivuko Kimoja kufanya kazi na kushindwa kumudu kupunguza msongamano huo.
Baadhi ya wananchi waliokwama wamekiambia kituo hiki kwamba hata kivuko hicho kikubwa kilipoanza kazi kilizidiwa kutokana na muda wa asubuhi kuwa na idadi kubwa ya watu na magari wanaovuka kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine kama inavyoonekana.
Hali hiyo imemlazimisha Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Dakta FAUSTINE NDUNGULILE kuitaka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kukifanyia ukarabati Kivuko cha MV Magogoni ili kisilete maafa kwa wananchi wanaokitumia hasa baada ya kuwa kibovu kwa muda mrefu.
Katika taarifa yake Dakta NDUNGULILE amesema amekuwa akipokea malalamiko ya wananchi wa Kigamboni wanaodai kwamba kivuko hicho ni kibovu na huchukua muda wa zaidi ya nusu saa kuvuka kati ya Kigamboni na Feri ambapo asubuhi ya Alhamisi Februari 11 kilipoteza mwelekeo na kusababisha taharuki kubwa.
Aidha Dakta NDUNGULILE amesema wananchi hao wamedai kuwa injini za kivuko hicho zimekuwa zikizima mara kwa mara na kukifanya wakati mwingine kipoteze mwelekeo kikiwa majini kama ilivyotokea Februari 10 mwaka huu na ambapo kivuko hicho kilipoteza mwelekeo na kuelekea Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere
Amesema kutokana na malalamiko hayo yeye kama Mbunge ameamua kumwandikia Barua ya tatu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kumkumbusha barua ya awali yenye kumbukumbu no KIG/FER/VOL.ya Januari Mosi Mwaka huu inayoeleza kutoridhishwa na huduma za Kivuko cha Kigamboni na kuitaka wizara kuchukua hatua mara moja kwani tangu barua hiyo ilipowasilishwa hakuna jitihada zilizoonekana za kuondoa adha inayowakabili wananchi wa Kigamboni.
Mashuhuda wanadai kuwa vilio na kelele zilisikika pale maji yalipoanza kupanda ndani ya kivuko kutokana na kuzidiwa na idadi ya watu wakati kivuko hicho kikubwa kilipoanza tena kufanya kazi hali iliyowafanya abiria waanze kujitosa ndani ya maji kwa wale wanaojua kuogelea.
***
Editha Mayemba